Uhaba wa mbolea duniani unaongeza bei ya chakula na kuziacha nchi maskini zikikabiliwa na mgogoro, anasema bosi wa kampuni kubwa ya mbolea. Svein Tore Holsether, mtendaji mkuu wa Yara International, aliiambia BBC bei ya juu ya gesi ilikuwa ikipandisha gharama ya mbolea na kuathiri bei ya chakula duniani kote.
Mbolea inahitaji kiasi kikubwa cha gesi katika uzalishaji wake. Bw Holsether alisema kampuni ya Yara imelazimika kupunguza kiasi cha uzalishaji kutokana na bei ya juu ya gesi, jambo ambalo limesababisha uhaba.
Mtendaji mkuu huyo alisema nchi zinazoendelea zitaathirika zaidi na uhaba huo, huku mavuno ya mazao yakipungua na chakula bei kupanda.
"Inatisha sana, tunakabiliwa na shida ya chakula na watu walio hatarini wanapigwa vibaya sana," aliambia kipindi cha Leo cha BBC. "Inaathiri bei ya chakula kote ulimwenguni na inagusa pochi za watu wengi. Lakini kwa baadhi ya watu, hasa katika nchi zinazoendelea, hili si swali tu kuhusu pochi, bali ni suala la maisha au kifo.”